Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2018

SOMO # 02: MSAMAHA

Mpendwa nakusalimu katika jina la Yesu Kristo. Mpedwa hakuna mtu aliyekamilika kila mtu anamadhaifu katika maisha , kutokana na kuwa tunamadhaifu mengi ,kwahiyo kukoseana/kutofautiana ni lazima kuwepo tu. Kwa minajili hiyo ni lazima sasa tuweze kuachilia msamaha kwa wale wanaotukosea au tuliowakosea kuwaomba msamaha ili Mungu nasi aweze kutusamehe makosa yetu. Maana katika MATHAYO 6:14-15 imeandikwa;- 14 . Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. 15 . Bali msipowasamehe watu makosa yao na Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu. Mpendwa hayo maneno kutoka Mathayo sio mageni kwako wala neno msamaha sio geni kwako, tambua kuwa neno msamaha linamaana kubwa sana katika maisha yetu ili kuboresha upendo baina yetu sisi na mbele za Mungu. Pia katika MARKO 11:25-26 imeandikwa;- 25 . Ninyi kila msimamapo na kusali sameheni mkiwa na neno juu ya mtu ili na Baba yenu aliye mbinguni awasemehe na ninyi makosa yenu. 26 . Lakini kama nin...

SOMO # 01: ADUI

 BWANA YESU ASIFIWE MPENDWA Mpendwa bila shaka u mzma wa afya kama hali sio nzuri basi Bwana atakuponya tu. Nakukaribisha katika somo hili Somo linatoka katika kitabu cha ZABURI 143:9 kama ilivyoandikwa;- Ee Bwana uniponye na adui zangu nimekukimbilia wewe unifiche. Mpendwa tumezungukwa na maadui wengi sana katika Maisha yetu, maadui hao tunaishi nayo na wengine hawaonekani kwa macho yetu. Je utamjuaje adui yako??? Zifuatazo ni sifa 15 za aliye adui yako, ukiziona hizo jua tu huyo ni adui wako pasipo hata kuuliza. 1. Anayekuwazia mabaya ,huyo ni adui yako. 2. Anayekusengenya ,huyo ni adui yako. 3. Anayekuchukia bila sababu,huyo ni adui yako. 4. Anayekugombanisha na watu,huyo ni adui yako. 5. Anayekusema mabaya ,huyo ni adui yako. 6. Anayetaka usiolewe/ usiowe, huyo ni adui yako. 7. Anayetaka uanguke kiimani au huduma yako ife, huyo ni adui yako. 8. Anayetaka ufe siku yoyote, huyo ni adui yako. 9. Anayetaka upate ajali, huyo ni adui yako. 10. Anayetaka biashar...