Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2023
 SOMO # 18:  SOMO: ITAMBUE MAANA HALISI YA KUMPENDA MUNGU Utangulizi: Watu wengi sana wamekuwa wakisema wanampenda Mungu lakini ukiangalia uhalisia wa maisha wanayoyaishi na wanachokiongea inakuwa ni tofauti kabisa. Mtu anasema anampenda/anamheshimu Mungu lakini ukiingalia moyo wake upo mbali naye kutokana na matendo mabaya anayoyatenda kama ilivyoandikwa katika kitabu cha MATHAYO 15:8-9 kwamba; 8. Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali name, 9. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu. Vile vile imeandikwa katika kitabu cha ISAYA 23:13-15 kwamba; 13. Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walicho nacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa; 14. kwa sababu hiyo mimi nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, kazi ya ajabu na mwujiza; na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa. 15. Ole wao...
  SOMO # 13: FURAHA ISIYO NA UKOMO Heri ya mwaka mpya Wapendwa! Wapendwa siku zote katika Maisha haya tunayoishi hapa duniani wakati mwingine huwa tunapitia changamoto nyingi sana mpaka zinapelekea kukosa furaha kwa kipindi furani, baada ya kusahau furaha hurudi tena. Lakini siku ya leo Mungu anatuambia katika kitabu cha 1 Wathesalonike 5:16 kwamba;- Furahini siku zote .   Neno hilo ‘Furahini siku zote’ lina maana kubwa sana katika Maisha yetu endapo kama tutalichukulia kwa uzito mkubwa sana. Mungu kusema hivyo sio kwamba hajui kama huwa wakati mwingine tunapata changamoto ambazo zinatuondolea furaha. Lakini Yeye anatamani tuzichukulie hizo changamoto kama ni sehemu ya Maisha kwani huwa zinamwisho kwahiyo zisituondolee furaha ndani ya mioyo yetu.   Mpendwa tambua kwamba Unapokuwa na Yesu kisawasawa ndani yako na ukapata changamoto inatakiwa usiiangalie hiyo changamoto maana itakuondolea furaha bali mwangalie Yesu ,yeye ndio ataiangalia hiyo changamoto na kuin...