SOMO # 11:  MKARIBIE MUNGU NAYE ATAKUKARIBIA HUU MWAKA 2021

Yakobo 4:8 imeandikwa;- Mkaribieni Mungu naye atawakaribia. Itakaseni mikono yenu enyi wenye dhambi ,na kuisafisha mioyo yenu enyi wenye nia mbili.

Mpendwa natumaini u mzima wa afya kabisa, na unaendelea vizuri na majukumu yako kama kawaida.

Kabla sijaendelea naomba kukuuliza hili swali ndugu mpendwa unayesoma ujumbe huu.

Je! Ni mambo ngani upo nayo karibu toka huu mwaka uanze?? Je! Ni Mazuri au Mabaya??

Mpendwa Mungu anatukumbusha siku hii ya leo tugeuke kwa kutoka kule ambapo tumekuwa karibu na Mambo mabaya ambayo yanatupekelea kubaya,  kwa sababu mambo hayo yataharibu maisha yetu kabisa.

Ukiwa karibu na Mungu siku zote naye atakuwa karibu na wewe kwa kila jambo ambalo utakuwa unalitenda , utakalolihitaji na hata kwa mambo utakayoyapitia yawe mabaya au mazuri lazima Mungu atakuwa pamoja na wewe.

Mpendwa usiwe karibu na dhambi , itakupeleka pabaya

1.   Usiwe karibu na Ulevi ,bali Kuwa karibu na Mungu naye atafanya mambo makubwa katika maisha yako.

2.   Usiwe karibu na Uzinzi maana utaishia pabaya mpendwa, bali Kuwa karibu na Mungu naye atafanya mambo makubwa katika maisha yako.

3.   Usiwe karibu na marafiki wabaya maana watakupeleka pabaya, bali Kuwa karibu na Mungu naye atafanya mambo makubwa katika maisha yako.

4.   Usiwe karibu na Wavivu huu mwaka maana na wewe utaishia kuwa mvivu tuu ,hatimaye hutaweza kutimiza lengo lako hata moja kwa huu mwaka.

5.   Usiwe karibu na watu wenye kukatisha tamaa ,maana na wewe utakata tamaa kwa baadhi ya mambo uliyopanga kuyatekeleza huu mwaka.

6.   Usiwe karibu na watu matapeli,waongo,wafitinishaji,n.k  maana na wewe utaishia kuwa hivyo tu.

Mpendwa kuwa karibu na Mungu maana yake ni kumwamini na kumtumikia Yeye, mpendwa hutajuta hata siku moja kuwa ndani ya Yesu.

Kuwa ndani ya Yesu kuna faida kubwa sana wala hakuna hasara yoyote, bali kuwa ndani ya shetani hakuna faida hata moja vyote ni ubatili mtupu, usidanganyike na mambo ya muda mfupi tu ambayo mwisho wake ni mbaya mnoo.

Unapokuwa mbali na Mungu na Yeye anakuwa mbali na wewe, unapokuwa karibu na shetani naye anakuwa karibu na wewe . Mpendwa chagua kuwa karibu na Mungu.

Kusudia kugeuka(Tubu)  kuanzia sasa na umfate Bwana Yesu kuwa ndiyo mwokozi wa maisha yako( Ufunuo 2:5 imeandikwa;- Basi kumbuka ni wapi ulipoanguka  ukatubu, uyafanye matendo ya kwanza. Lakini usipofanya hivyo ,naja kwako nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake usipotubu.

Ubarikiwe sana mpendwa

@Msufu-January 21, 2021 www.msufu.blogspot.com

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

SOMO # 03: MAAJABU YA NAMBA SABA

SOMO # 01: ADUI

SOMO # 07: MAOMBI