SOMO # 8:    USILAUMU SONGA MBELE MWAKA 2021

Mpendwa kwanza na kusalimu kwa Jina la Yesu Kristo.

Kwanza ni jambo la kumshukuru Mungu sana  kwa kutupa neema ya kuanza mwaka huu 2020 tukiwa wazima toka umeanza mwezi wa kwanza na sasa tupo mwezi wa 12 mwishoni kabisa , haijalishi uliweka MALENGO mengi kiasi gani mwaka huu, na mengine yametimia au hayajatimia mpaka muda huu unapoelekea mwisho wa mwaka au hukuweka Malengo kabisa,Mpendwa usilaumu wala usikate tamaa maana katika kitabu cha MHUBIRI 3:1 imeandikwa kwamba;- Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya Mbingu. Hivyo basi unapoona malengo yako hayajatimia jua kwamba wakati na majira yake utafika tu na malengo mpaka yatatima katika jina la Yesu Kristo.

Mpendwa unaweza ukatafakari, kwa huu mwaka 2020 umefanya jambo gani la maana na unaweza usipate majibu, lakini nakutia moyo kwamba usijilaumu kwa kupoteza muda mpaka mwaka unaenda kuisha bado kuna vitu hujavifanya, lakini tambua kwamba mwaka 2021 ndiyo huo unakuja hivyo basi weka MALENGO yako na uyaombee, Mungu atayatakabali.

Inawezekana uliweka malengo yako vizuri kabisa mwaka huu 2020 lakini ikatokea ukapata changamoto ya kiafya labda mpaka sasa unaumwa , au yakifedha au migogoro ikatokea au ukakosa shauku kabisa ya kutekeleza malengo yako, mpendwa nataka kukwambia kwamba endelea kumtumainia Mungu wala usikate tama kwa kulaumu( ZABURI 125:1 imeandikwa;- Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni ambao hautatikisika, wakaa milele) ninakuombea mwaka 2021 Mungu akakushangaze katika jina la Yesu Kristo, maana mawazo anayo kuwazia wewe ni mawazo mema kabisa wala sio mabaya kama ilivyoandikwa katika kitabu cha YEREMIA 29:11 kwamba;- Maana nayajua mawazo ninayokuwawazia ninyi, asema Bwana ni mawazo ya amani wala si ya mabaya ,kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Vilevile unaweza ukawa uliweka  malengo yako lakini kuna watu(marafiki,majirani,ndugu n.k)  walikuja kukukatisha tamaa au mazingira uliyopo yalikukatisha tamaa na mpaka sasa hakuna ulichofanya au umefanya kidogo, mpendwa nataka kukwambia kwamba mwaka 2021 Mungu anaenda kukushangaza katika jina la Yesu Kristo.  Wewe endelea tu kumtumaini maana Yeye macho yake yapo kila mahali anakuona mpendwa wala usijali kwa kuhangaika kwako yaani umekata tamaa au umebaki kujilaumu tu tambua kuwa  neema ya Mungu bado ipo katika maisha yako( MITHALI 15:3 Macho ya Bwana yapo kila mahali yakimchunguza mbaya na mwema), lakni pia Biblia inasema katika ZABURI 23:6 kwamba;- Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu ,nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. Mpendwa nami ninakuombea katika jina la Yesu Kristo wema na fadhili za Bwana vikufuate mwaka 2021 popote ulipo wewe unayesoma ujumbe huu kama jinsi Neno lake Bwana linavyosema katika Zaburi 23:6 Amen.

Licha ya hivyo inawezekana  malengo uliyoyaweka mwaka huu 2020 hukuanza kwa kuyatanguliza mbele za Mungu yaani hukumkabidhi Mungu, ila ukaanza kuwaambia kwanza watu wako wa karibu hatimaye ndiyo ikafikia hatua ya Malengo yako kuvurugika kabisa na kukatishwa tamaa kukawa kwingi, yaani ikawa ni tofauti na ulivyotegemea wewe.

Nataka kukwambia kwamba MALENGO yako yote ya mwaka 2021 cha kwanza inatakiwa umkabidhi Bwana Yesu ili aweze kuyabariki , kuyalinda na kukutia Ujasiri na Nguvu unapokwenda kuyatekeleza  katika huo mwaka mpya (ZABURI 37:5 imeandikwa;- Umkabishi Bwana njia yako, pia umtumaini naye atafanya.)

Mpendwa kama tulivyouona huo mstari kutoka Zaburi 37:5 kwamba Mungu anaposema umkabidhi NJIA YAKO, maana yake kwamba NJIA ndio mambo( MALENGO) yako yote unayotaka kuyafanya cha kwanza inatakiwa uyapeleke mbele za Mungu ili yakapate kibali ( ZABURI 19:14 imeandikwa;- Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu yapate kibali mbele zako, Ee Bwana mwamba wangu na mwokozi wangu. ) Usianze kwanza kuwaambia watu malengo yako kabla hujayakabidhi mbele za Mungu, kama hutaanza kumkabidhi Mungu hapo ndipo shetani atakapopata nafasi ya kuyakwamisha malengo yako maana hukuanza kwanza kwa kumkabidhi Mungu.

Mpendwa nimalizie kwa kusema hivi, kuweka MALENGO( yaani ya muda mrefu na mfupi)  katika maisha yako ni jambo la muhimu sana maana hata Mungu alipokuwa anaumba dunia na vitu vyote vilivyomo ndani yake aliweka malengo kwanza kabla ya Kuumba maana hakukurupuka tu , ndiyo maana ukisoma katika kitabu cha MWANZO 1: 1-31 na 2:1-2  utaona kwamba Mungu alitumia siku 7(wiki moja) kutimiza  MALENGO yake aliyokuwa ameyapanga na kweli yakatimia ,ukisoma kwa makini mistari hiyo kutoka kitabu cha Mwanzo utaelewa ninachokizungumzia.

MHIMU: Kabla ya kuweka MALENGO yako  ya mwaka 2021 zingatia haya mambo sita(6);

 

 


Ubarikiwe sana mpendwa.

@Msufu- Desemba 29, 2020, www.msufu.blogspot.com, 0753255132

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

SOMO # 03: MAAJABU YA NAMBA SABA

SOMO # 01: ADUI

SOMO # 07: MAOMBI