SOMO #9: MAMBO MUHIMU YA KUYAFANYA KABLA YA KUINGIA
MWAKA MPYA 2021.
Mpendwa karibu ujifunze somo hili.
1.
Mshukuru
Mungu kwa yote aliyokutendea na ambayo hajayatenda huu mwaka 2020
1
Wathesalonike 5:18 imeandikwa;- Shukuruni kwa kila jambo ;
maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
1
Mambo ya Nyakati 16:34 imeandikwa;- Mshukuruni Bwana kwa
kuwa ni mwema kwa maana fadhili zake ni za milele
Zaburi
75:1
imeandikwa;- Ee Mungu twakushukuru ,twakushukuru kwa kuwa jina lako li karibu
,watu huyasimuliya matendo yako ya ajabu.
Mpendwa, kwahiyo upate au usipate yote hayo ni
mapenzi ya Mungu ,hivyo basi Mshukuru kwa vyote.
Baadhi
ya Mambo ya kushukuru mbele za Mungu ni kama yafuatayo;-
i.
Kuna mambo Mungu amefanikisha kukutendea
ambayo yalikuwa yapo ndani ya malengo yako ya 2020
ii.
Kuna mambo amakufanyia ambayo hayakuwepo
ndani ya malengo yako ya Huu mwaka 2020.
iii.
Kuna mambo ambayo amekutendea ambayo
hayaonekani kwa macho yako Huu mwaka 2020. Mfano Mungu amekuepusha na mambo
mabaya mengi sana bila wewe kujua wala kuona kwa macho yako ,kama vile
amekupigania na Wachawi na kakuepusha na mitengo ya wachawi bila ya wewe kujua
kabisa.
iv.
Mshukuru Mungu kwa ajili ya afya ulilonayo
maana hiyo ni Neema ya Mungu tu.
v.
Mshukuru Mungu kwa ajili ya Wazazi
wako,Ndugu zako,Marafiki zako n.k . Mwambie Mungu asante kwa ajili ya Familiya
yangu, Wazazi wangu, Walezi wangu,Ndugu zangu wote kwa ujumla n.k . Maana Mungu
pia amewatendea mambo makubwa huu mwaka 2020.
vi.
Mshukuru Mungu kwa ajili ya malengo
uliyoyaweka mwaka huu lakini bado hayajatimia au yamefikia hatua nzuri kabisa.
Mfano Ujenzi wa nyumba labda ulishaanza huu mwaka kujenga lakini bado hujamalizika,
au tayari ulianza kukusanya pesa kwa ajili ya kufanya jambo fulani na tayari
baadhi ya kiasi cha pesa upo nacho.
vii.
Mshukuru Mungu kwa neema ya Wokovu
aliyokupa na umeendelea kusimama na wokovu huo mpaka huu mwaka unapokwenda
kuisha leo hii. Hiyo ni neema sema Yesu asante Mshukuru Mungu katika roho na
kweli
2.
Kusamehe
waliokukosea na wewe kuwaomba msamaha uliowakosea.
MATHAYO
6:14-15 imeandikwa;-
14.Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na
Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.
15. Bali msipowasamehe watu makosa yao
na Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
MARKO
11:25-26 imeandikwa;-
25.Ninyi kila msimamapo na kusali sameheni
mkiwa na neno juu ya mtu ili na Baba yenu aliye mbinguni awasemehe na ninyi
makosa yenu.
26. Lakini kama ninyi hamsamehe wala
Baba yenu aliye mbinguni hata wasamehe ninyi makosa yenu.
Mpendwa usipende kuingia
mwaka mpya huku unakinyongo na mtu au mtu anakinyongo na wewe , Mungu anasema
unaposamehe na wewe ndiyo utasamehewa na Yeye , bali usiposamehe na Yeye hata
kusamehe, sasa niambie ni nani ambaye hataki kusamehewa na Mungu? Basi wewe
utakuwa ni malaika yaani humkosei Mungu, kwahiyo huna haja ya kumwomba msamaha.
Msamaha unaleta afya ya
kiakili pia na ya kimwili, vile vile unakuweka wewe kuwa huru muda wote, kwa
sababu moyo wako unakuwa hauna malimbikizo ya makosa yoyote ju ya watu
waliokukosea.
Mpendwa tunaishi kwenye
jamii ya watu wengi hivyo basi kukoseana ni lazima kutokee, hivyo basi msamaha
ni endelevu kwa sababu leo atakukosea huyo kesho atakukosea tena mwingine n.k..
Msamaha unaendana na
kujishusha, yaani ni lazima mmoja ashuke ili kuweka mambo sawa. Hakikisha
unaingia 2021 moyo wako upo safi.
3.
Tubu
dhambi zako zote.
Isaya
1:18
imeandikwa;- Haya njooni tusemezane asema Bwana,dhambi zenu zijapokuwa nyekundu
sana ,zitakuwa nyeupe kama theluji ,zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakuwa
kama sufu.
1
Yohana 1: 8-10 imeandikwa;-
8. Tukisema kwamba hatuna dhambi twajidanganya
wenyewe ,wala kweli haimo kwetu.
9. Tukiziungama dhambi zetu Yeye ni mwaminifu na wa
haki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote
10. Tukisema kwamba hatukutenda dhambi ,twamfanya
Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.
Warumi
3:23
imeandikwa;- Kwa sababu wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa
Mungu.
Mpendwa hakikisha unamwomba Mungu akutakase dhambi
zako zote ili mwaka mpya uingie ukiwa safi kabisa
4.
Fanya
tathmini ya mwaka mzima huu unaoisha leo.
i. Kama ni mfanaya biashara, hebu jaribu
kuitathimini biashara yako huu mwaka kama kuna mahali pa kujirekebisha, basi
mwaka 2021 ndio uwe mpya wenye mafanikio
ya biashara yako, au kama ulianzisha biashara na ikafa basi jaribu kuangalia ni
kitu kipi kilisababisha biashara ife ili mwaka 2021 ukaifufue biashara yako kwa
ushindi mkubwa, au ukaanzishe na nyingine kabisa.
ii. Kama wewe
ni mfanyakazi umeajiriwa au umeajiajiri au wewe ndio umeajiri, hebu fanya
tathimini uone je huwa unafanya kazi kwa kujituma au mpaka ulazimishwe lakini
unapenda mshahara? Je huwa unawahi kazini kulingana na muda wa kazi uliowekwa
kwenye taasisi yako?. Je mahusiano yako yapoje na wafanyakazi wenzako? Kama ni
mabaya basi jitahidi mwaka 2021 uanze mambo mapya kwa kuwa na mahusiano mazuri
na wafanyakazi wenzako. Kama wewe ni boss wa ofisi fulani je unawaongoza vipi
watu wako wa chini? Unawanyima haki au huwajali kabisa au unajali mambo yako
tu? Kama kuna mahali huendi vizuri basi 2021 ujirekebishe katika jina la Yesu
Kristo.
iii. Kama
wewe ni mwanandoa , tathimini ndoa yako je unaishi vipi na mwenzi wako ? kama
kuna mahali hamuelewani na mwenzi wako wa ndoa hebu kaeni chini myaweke mambo
sawa ili 2021 iwakute mpo na furaha tele . Msijilimbikizie makosa kwenye ndoa
yenu maana haitaleta afya katika ndoa ila migogoro ndio itazidi zaidi hatimaye
ndoa itayumbayumba mnoo.
iv. Kama wewe
ni mwanafunzi, hebu jitathimini kwenye masomo yako je huwa unafanya vizuri au
vibaya kwenye mitihani? Kama ni vibaya angalia sababu za kutokufaulu vizuri ni
zipi halafu ujilekebishe mwaka 2021 uanze kwa kishindo kikubwa sanaaa. Labda
huwa unachelewa kwenye vipindi au huudhurii darasani au hufanyi test,quiz au
assignments n.k ..vyote hivyo ujirekebishe mpendwa yaani uwe mtu mpya mwaka 2021.
v. Kama wewe
ni mtumishi wa Mungu labda Mhubiri au mwimbaji n.k ,hebu jitathimini huu mwaka
2020 umefanya huduma kwelikweli ya kumtumikia Mungu kwenye nafasi yako?( Yeremia 48:10A imeandikwa;- Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa
ulegevu Jichunguze wewe uliyeokoka mahusiano yako na Mungu yakoje? Ili
mwaka 2021 uweze kuwa karibu na Munggu zaidi.
vi. Fanya
tathimini kwenye Mahusiano yako wewe na
ndugu zako je yapoje? Pia na Marafiki
zako, wafanyakazi wenzako,Majirani zako,Wafanya biashara wenzako n.k..Kama
kwenye familiya yenu kuna migogoro au kwenye ukoo wenu basi hakikisha wewe
unayeusoma ujumbe huu ukawe chanzo cha kuhakikisha amani inapatikana, ili
ugomvi uweze kuisha hatimaye mwaka 2021 muingie mkiwa wapya kabisa yaani
mnafurahiana ndugu wote na wala kusiwe na matabaka yoyote.
5.
Weka
malengo
Mpendwa hakikisha unaingia mwaka 2021 tayari ukiwa
na malengo mapya kabisa ambayo ndiyo utakwenda kuyatekeleza.
Kuingia mwaka 2021 bila malengo inakuwa ni kama vile
umeianza safari ambayo hujui unakokwenda ni wapi na utafika lini, mwisho wake
mwaka unaisha hamna hata kitu cha maana ulichofanya, kwa sababu itakuwa
unafanya hiki mara ufanye kile, mwisho wake unajikuta hakuna ulichokitimiza na
mwaka unakuwa umeisha.
Kama upo kwenye ndoa, malengo mpange wote wawili sio
mtu mmoja , na kila mtu ayafahamu malengo ili kama kuna mtu mmojawapo anataka
kufuja pesa unamkumbusha mume wangu/mke wangu lakini kumbuka malengo
tuliyoyaweka, kwa jinsi pesa zinavyotumika hivyo inaweza kupelekea tukashindwa
kufikia malengo yetu. Lakini kama malengo yakiwekwa na mtu mmoja uwajibikaji
nakuwa mdogo kwa mtu asiyeyafahamu wala hakushirikishwa kwenye kuyapanga
malengo hayo.
Lakini kama kuna malengo ambayo hayajamalizika
kutekelezeka mwaka huu 2020 basi ya bebe ukayatekeleze mwaka 2020.
Unapoweka malengo weka na mikakakati(strategies) ya
kutekeleza malengo hayo, pia weka muda mwafaka(time frame) wa kila lengo
kuhakikisha umelitimiza ndani ya muda huo. Mfano umeweka lengo la kuanza ujenzi
2021, kwahiyo labda unapanga kuanzia mwezi fulani nitafanya hivi, na kuanzia
mwezi Fulani nitafanya hivi, vivyo hivyo mpaka mwaka unaisha kunakuta umetimiza
kabisa.
6.
Jitabirie mafanikio na mambo mazuri wala sio mabaya mwaka 2021.
Yakobo
3:10
imeandikwa;- Katika kinywa kilekile
hutoka Baraka na laana, ndugu zangu haifai mambo hayo kuwa hivyo.
Mithali
18:21 imeandikwa;- Mauti na uzima huwa katika uwezo wa
ulimi ,na wao waupendao watakula matunda yake.
Hivyo basi mpendwa kutokana na mistari hiyo utaona
kwamba wewe uwezo wa kujitabiria mabaya au mazuri upo ndani ya uwezo wako , maana kinywa
kinaumba jambo, mfano kama wewe kila siku ni wa kusema mimi siwezi na kweli
utakuwa huwezi maana unakuwa umejiumbia mwenyewe. Mungu alipokuwa unaumba dunia
kwanza alitamka kwa kinywa chake na kweli ikawa katika uhalisia, mfano ukisoma
kitabu cha Mwanzo 1:6 utaona uhalisia
ninao uzungumza ambapo imeandikwa kwamba;- Mungu akasema na liwe anga katikati
ya maji ,likayatenge maji na maji.
Mungu alivyotamka ndivyo ilivyokuwa , hivyo hivyo na
kwako pia utakavyojitamkia kwa kinywa chako ndivyo utakavyokuwa. Mpendwa
jitabirie mambo yaliyomema mwaka 2021 hakika utaona uhalisia wake.
Ubarikiwe
sana mpendwa, nakutakia maandalizi mema ya kuupokea mwaka mpya 2021.
@Msufu- Desemba 31, 2020, www.msufu.blogspot.com,
0753255132
Maoni
Chapisha Maoni